Search This Blog

SportsRaw

SportsRaw

Monday 17 October 2016

Ozil amtia kiwewe Wenger

Kocha wa The Gunners Arsene Wenger amesema anaamini kuungo fundi wa Ujerumani Mesut Ozil ataendelea kuwepo katika klabu hiyo licha ya mchezaji huyu mwenye asili ya Uturuki kutaka kulipwa pauni 200,000 kwa wiki.

Arsene Wenger remains coy over Mesut Ozil's contract but says 'it's not about money'
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger
Ili kumbakisha Ozil inabidi Arsenal ivunje benki ili kupata saini yake,jambo lingine litakalomfanya asaini mkataba huo ni lazima Arsenal ianze kushinda mataji, "hahitaji kushawishiwa anataka kubaki nasi, hela kwake sio tatizo" alisema Wenger

Tupo kwenye ligi yenye timu kama Manchester City Liverpool Tottenham, na Manchester United huwezi kuwa na uhakika wa kutwaa ubingwa kila mmoja anapigania nafasi hiyo,

Kwa sasa Ozil analipwa Pauni 140,000 kwa wiki na katika mchezo wa juzi dhidi ya Swansea city alifunga goli safi akimalizia krosi nzuri ilipigwa na Alexis Sanchez na siku hiyo alikuwa anashereheka kutimiza umri wa miaka  28 mkataba wa sasa utaisha 2018 kwa maana hiyo kuanzia dirisha la majira ya kiangazi atakuwa huru kuondoka.

Ozil netted a brilliant volley to put the Gunners ahead against Swansea on Saturday afternoon
 Mchezaji wa Arsenal (Kulia) Mesut Ozil akifunga goli kwenye mchezo wa ligi ya Epl dhidi ya Swansea City The Gunners walishinda 3-2. 

0 comments:

Post a Comment