Search This Blog

SportsRaw

SportsRaw

Sunday, 16 October 2016

Real, Atletico zafanya sherehe La Liga

Wakiwa kwenye kiwango kizuri mabingwa wa Ulaya Real  Madrid jana usiku walifanikiwa kupata ushindi dhidi ya Real Betis kwa kuifunga 1-6 ushindi huu umesitisha matokeo ya sare  nne mfululizo huku Madrid wakitandaza soka safi.

Ronaldo tries to find a route past Betis goalkeeper Antonio Adan at the Benito Villamarin



Wali droo dhidi ya Villarreal, Las Palmas, Borussia Dortmund na Eibar kocha Zinedine Zidane alikuwa kwenye presha kubwa ya kuhakikisha wanapata matokeo, baada ya mechi Zizuo alikiri hajawahi kuona timu yake inaanza mchezo kwa morali ya juu na kusema matatitzo ya kisaikolojia yalikuwa yanawasumbua vijana wake.

Beki aliechukua nafasi ya nahodha Sergio Ramos, ambaye ni majeruhi  Raphael Varane alianza kufungua ukurasa wa magoli  Karim Benzema akafunga la pili, beki wa kushoto Marcelo akaipatia la tatu,na kuungo mshambualiji Isco akifunga magoli mawili kabla Cristiano Ronaldo kuhitimisha karamu hiyo ya magoli kwa kuzifumania nyavu kwa mara ya sita

Isco (left) shares a high five with Pepe after the two combined for Real's fourth goal

Katika mechi nyingine Atletico Madrid walipata ushindi mnono wa magoli 7-1 walipokuwa nyumbani dhidi ya Granada magoli yalifungwa na Ferreira aliepiga hat-trick 34' 45' 61' Gaitan akafunga mawili  63'   81' dakika tatu baadae Correa alifunga nae 85 ' na Tiago akahitimisha la saba 87'.

kwa matokeo ya  jana Atletico Madrid na Real  Madrid wapo sawa kwa kfikisha pointi 18, wakwa kileleni na wanatofatiana magoli ya kufunga  nafasi ya tatu wapo Sevilla na 17 na Barcelona baada ya ushindi wa jana wanashikilia nafasi ya nne na pointi 16 katika La Liga.

Cristiano Ronaldo congratulates Marcelo for scoring Real Madrid's third at Real Betis

0 comments:

Post a Comment