Ligi Kuu soka Tanzania bara imeendelea leo Jumapili ya October 16 2016 katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, mabingwa watetezi wa Ligi hiyo Dar es Salaam Young Africans walikuwa wageni wa Azam FC katika mchezo huo ambao kila timu ilihitaji pointi tatu ili ijiweke katika nafas nzuri kwenye msimamo wa ligi.
timu zote mbili zilikingia kwa kumbukumbu kwa wenyeji Azam FC kufungwa goli 1-0 kweny mchezo mchezo uliopita dhidi ya Stand United, wakati wanajangwani walikuwa na kumbukumbu ya ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar mechi iliopigwa katika uwanja wa Uhuru.
matokeo hayo yanaifanya Azam FC iendelee kushika nafasi ya saba wakiwa na pointi 12 baada ya kushuka ndimbani mara tisa na Yangu katika nafasi ya tatu wajiwa na pointi 15 wakiwa wamecheza mara nane, Simba bado wanaongoza ligi kwa pointi 23 baada ya michezo tisa
0 comments:
Post a Comment