Search This Blog

SportsRaw

SportsRaw

Saturday, 15 October 2016

VPL kutimua vumbi leo

Ligi Kuu Bara inatarajiwa kuendelea leo Jumamosi kwa michezo mitatu mnyama Simba anayeongoza katika msimamo wa  ligi itaikaribisha Kagera Sugar  kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Image result for chirwa yanga 2016

Mchezo mwingine utakuwa ni kati ya JKT Ruvu na Mwadui ya Shinyanga mchezo  utakaofayika Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani ambako utachezeshwa na Mwanamama mwamzi mwenye beji la FIFA, Mwanahamisi Matiku wa Dar es Salaam.

Stand United ya Shinyanya itaikaribisha African Lyon kwenye Uwanja wa CCM Kambarage katika mchezo .

Ligi hiyo itaendelea kesho  Jumapili kwa mchezo utakaozikutanisha timu za Azam na Young Africans; zote za Dar es Salaam. Mwamuzi wa mchezo huo atakuwa Israel Nkongo wa Dar es Salaam. 

 Ruvu Shooting na Mbeya City Jumapili watatoana jasho kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani. 

Mtibwa Sugar ya Morogoro na Tanzania Prisons ya Mbeya nazo zitacheza Jumapili Oktoba 16 kwenye Uwanja wa Manungu mkoani Morogoro. .

 Toto African ya mwanza dhidi ya Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. 

0 comments:

Post a Comment